-
Nehemia 2:19, 20Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
19 Sasa Sanbalati Mhoroni, Tobia+ ofisa* Mwamoni,+ na Geshemu Mwarabu+ waliposikia jambo hilo, wakaanza kutudhihaki+ na kutudharau wakisema: “Mnafanya nini? Je, mnamwasi mfalme?”+ 20 Lakini nikawajibu: “Mungu wa mbinguni, Ndiye atakayetufanikisha,+ nasi watumishi wake tutasimama na kujenga; lakini ninyi hamna fungu wala haki ya kudai chochote wala kumbukumbu* katika Yerusalemu.”+
-