-
Ezra 4:1-3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 Maadui wa Yuda na Benjamini+ waliposikia kwamba watu waliorudi kutoka uhamishoni+ walikuwa wakimjengea hekalu Yehova Mungu wa Israeli, 2 mara moja wakamfikia Zerubabeli na viongozi wa koo* na kuwaambia: “Acheni tujenge pamoja nanyi; kwa maana, sisi pia tunamwabudu* Mungu wenu+ na tumekuwa tukimtolea dhabihu tangu siku za Mfalme Esar-hadoni+ wa Ashuru, aliyetuleta hapa.”+ 3 Hata hivyo, Zerubabeli na Yeshua na viongozi wa koo* za Israeli wakawaambia: “Hamna haki ya kujenga pamoja nasi nyumba ya Mungu wetu,+ kwa maana sisi wenyewe tutamjengea Yehova Mungu wa Israeli, kama alivyotuamuru Mfalme Koreshi, mfalme wa Uajemi.”+
-