Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Mambo ya Nyakati 36:23
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 23 “Mfalme Koreshi wa Uajemi anasema hivi: ‘Yehova Mungu wa mbinguni amenipa falme zote za dunia,+ naye ameniagiza nimjengee nyumba Yerusalemu, nchini Yuda.+ Yeyote miongoni mwenu, ninyi watu wake wote, Yehova Mungu wake na awe pamoja naye, na apande kwenda huko.’”+

  • Ezra 1:1-3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 1 Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Mfalme Koreshi+ wa Uajemi, ili neno la Yehova lililosemwa na Yeremia+ litimie, Yehova aliichochea roho ya Mfalme Koreshi wa Uajemi atoe tangazo katika ufalme wake wote, ambalo pia aliliandika,+ akisema:

      2 “Mfalme Koreshi wa Uajemi anasema hivi: ‘Yehova Mungu wa mbinguni amenipa falme zote za dunia,+ naye ameniagiza nimjengee nyumba Yerusalemu, nchini Yuda.+ 3 Yeyote miongoni mwenu, ninyi watu wake wote, Mungu wake na awe pamoja naye, na apande kwenda Yerusalemu, kule Yuda, na kuijenga upya nyumba ya Yehova Mungu wa Israeli—yeye ndiye Mungu wa kweli—ambaye nyumba yake ilikuwa Yerusalemu.*

  • Ezra 6:3, 4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 3 “Katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Mfalme Koreshi, Mfalme Koreshi alitoa agizo hili kuhusu nyumba ya Mungu huko Yerusalemu:+ ‘Nyumba hiyo na ijengwe upya iwe mahali watakapotolea dhabihu, na misingi yake inapaswa kuwekwa; kimo chake kiwe mikono 60,* upana wake mikono 60,+ 4 na iwe na safu tatu za mawe makubwa yaliyobingirishwa na kuwekwa mahali pake na safu moja ya mbao;+ na gharama zote zilipwe kutoka katika nyumba ya mfalme.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki