3Kuhani mkuu Eliashibu+ na ndugu zake makuhani wakaanza kujenga Lango la Kondoo.+ Wakalitakasa*+ na kuweka milango yake; wakalitakasa mpaka kwenye Mnara wa Mea,+ na mpaka kwenye Mnara wa Hananeli.+
6 Yoyada mwana wa Pasea na Meshulamu mwana wa Besodeya wakarekebisha Lango la Jiji la Kale;+ walilitengeneza kwa mbao, wakaweka milango yake, makomeo yake, na mapingo yake.
13 Hanuni na wakaaji wa Zanoa+ walirekebisha Lango la Bondeni;+ wakalijenga na kuweka milango yake, makomeo yake, na mapingo yake, pia walirekebisha sehemu ya ukuta yenye urefu wa mikono 1,000* mpaka kwenye Lango la Marundo ya Majivu.+