-
Nehemia 10:37, 38Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
37 Pia, unga wetu wa kwanza ambao haujakobolewa,+ michango yetu, matunda ya mti wa kila aina,+ divai mpya, na mafuta,+ tutawapelekea makuhani kwenye maghala* ya nyumba ya Mungu wetu,+ pia tutawapa Walawi sehemu ya kumi ya mazao ya mashamba yetu,+ kwa maana Walawi ndio wanaokusanya sehemu za kumi za mazao katika miji yetu yote ya kilimo.
38 Na kuhani, mwana wa Haruni, anapaswa kuwa pamoja na Walawi wanapokusanya sehemu ya kumi; Walawi nao wanapaswa kuleta sehemu ya kumi ya ile sehemu ya kumi katika nyumba ya Mungu wetu,+ kwenye vyumba vya* ghala.
-