-
Esta 4:1-3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 Mordekai+ alipojua mambo yote yaliyofanywa+ akayararua mavazi yake, akavaa nguo za magunia na kujimwagia majivu. Kisha akaenda katikati ya jiji, akilia kwa sauti kubwa na kwa uchungu. 2 Akaenda karibu na lango la mfalme, kwa maana hakuna mtu aliyepaswa kuingia katika lango la mfalme akiwa amevaa nguo za magunia. 3 Katika kila mkoa*+ ambako neno la mfalme na amri yake ilifika, kulikuwa na maombolezo makubwa miongoni mwa Wayahudi, pia walifunga,+ wakalia, na kuomboleza. Wengi wao walilala chini katika majivu wakiwa wamevaa nguo za magunia.+
-