-
Esta 8:11, 12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Katika barua hizo mfalme aliwaruhusu Wayahudi katika majiji yote wakusanyike ili walinde uhai wao* na kuangamiza, kuua, na kuharibu jeshi lolote la taifa lolote au mkoa* ambao huenda ungewashambulia wao, kutia ndani wanawake na watoto wao, na kuchukua mali zao.+ 12 Wangefanya hivyo siku ileile katika mikoa yote ya* Mfalme Ahasuero, siku ya 13 ya mwezi wa 12, yaani, mwezi wa Adari.*+
-