Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 20:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 7 “Usilitumie jina langu mimi, Yehova Mungu wako, kwa njia isiyofaa,+ kwa maana mimi, Yehova, sitakosa kumwadhibu yule anayelitumia jina langu kwa njia isiyofaa.+

  • Ayubu 4:18-20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Tazama! Hana imani na watumishi wake,

      Naye huona kwamba malaika* wake wana kasoro.

      19 Sembuse wale wanaokaa katika nyumba za udongo,

      Ambao msingi wao umo mavumbini,+

      Wanaopondwa kwa urahisi kama nondo!*

      20 Wanapondwa kabisa kuanzia asubuhi mpaka jioni;

      Wanaangamia milele, na hakuna yeyote anayetambua hilo.

  • Ayubu 22:2, 3
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  2 “Je, mwanadamu anaweza kuwa na faida kwa Mungu?

      Je, mtu yeyote mwenye ufahamu anaweza kuwa na faida kwake?+

       3 Je, Mweza-Yote anajali* kwamba wewe ni mwadilifu,

      Au je, anapata faida yoyote kwa sababu unafuata njia ya utimilifu?+

  • Ayubu 25:5, 6
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  5 Hata mwezi si mwangavu

      Na nyota si safi machoni pake,

       6 Sembuse mwanadamu anayeweza kufa ambaye ni buu,

      Na binadamu ambaye ni mnyoo!”

  • Ayubu 42:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 8 Sasa chukueni ng’ombe dume saba na kondoo dume saba kisha mwende kwa mtumishi wangu Ayubu, na mtoe dhabihu ya kuteketezwa kwa ajili yenu. Na mtumishi wangu Ayubu atasali kwa ajili yenu.+ Kwa hakika nitakubali ombi lake* nami sitawatendea kulingana na upumbavu wenu, kwa sababu hamkusema ukweli kunihusu kama alivyofanya mtumishi wangu Ayubu.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki