Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 23:31
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 31 “Nitaweka mpaka wenu kuanzia Bahari Nyekundu mpaka bahari ya Wafilisti na kuanzia nyikani mpaka kwenye Mto Efrati;+ kwa maana nitawatia wakaaji wa nchi hiyo mikononi mwenu, nanyi mtawafukuza kutoka mbele yenu.+

  • 1 Wafalme 4:21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Sulemani alitawala falme zote kuanzia Mto Efrati+ mpaka nchi ya Wafilisti hadi kwenye mpaka wa Misri. Walimletea Sulemani ushuru na kumtumikia siku zote za maisha yake.+

  • Zaburi 2:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  8 Niombe, nami nitakupa mataifa kuwa urithi wako

      Na miisho ya dunia kuwa miliki yako.+

  • Zaburi 22:27, 28
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Miisho yote ya dunia itakumbuka na kumgeukia Yehova.

      Familia zote za mataifa zitainama chini mbele zako.+

      28 Kwa maana ufalme ni wa Yehova;+

      Anayatawala mataifa.

  • Danieli 2:35
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 35 Wakati huo kile chuma, ule udongo wa mfinyanzi, ile shaba, ile fedha, na ile dhahabu, vyote pamoja, vikapondwapondwa na kuwa kama makapi kutoka kwenye uwanja wa kupuria wakati wa kiangazi, kisha upepo ukavipeperusha mbali hivi kwamba hakuna chembe yoyote ya vitu hivyo ingeweza kupatikana. Lakini lile jiwe lililoipiga ile sanamu likawa mlima mkubwa, nalo likaijaza dunia yote.

  • Zekaria 9:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Nitaondoa gari la vita Efraimu

      Na farasi kutoka Yerusalemu.

      Upinde wa vita utachukuliwa.

      Naye atatangaza amani kwa mataifa;+

      Utawala wake utaenea kutoka bahari mpaka bahari

      Na kutoka Mto Efrati mpaka kwenye miisho ya dunia.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki