-
Kumbukumbu la Torati 29:19, 20Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
19 “Lakini mtu akisikia maneno ya kiapo hiki na kujigamba moyoni mwake akisema, ‘Nitakuwa na amani, ingawa ninasisitiza kwamba nitaendelea kutembea katika njia za moyo wangu mwenyewe,’ na hivyo kuharibu kila kitu* kilicho kwenye njia yake, 20 Yehova hatakuwa tayari kumsamehe.+ Badala yake, hasira kali ya Yehova itawaka dhidi ya mtu huyo, na laana yote iliyoandikwa katika kitabu hiki hakika itampata,+ na Yehova kwa kweli atafutilia mbali jina la mtu huyo kutoka duniani.*
-