-
Danieli 3:29Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
29 Kwa hiyo ninaagiza kwamba watu wa kabila lolote, taifa, au lugha ambao watasema jambo lolote dhidi ya Mungu wa Shadraki, Meshaki, na Abednego, wanapaswa kukatwa vipandevipande, na nyumba zao zinapaswa kugeuzwa kuwa vyoo vya umma;* kwa maana hakuna mungu mwingine yeyote anayeweza kuokoa kama huyu.”+
-
-
Danieli 6:26, 27Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
26 Ninatoa agizo kwamba katika kila eneo la ufalme wangu, watu wanapaswa kutetemeka kwa woga mbele za Mungu wa Danieli.+ Kwa maana yeye ndiye Mungu aliye hai naye huishi milele. Ufalme wake hautaangamizwa kamwe, na utawala wake ni wa* milele.+ 27 Yeye huokoa,+ naye hufanya ishara na maajabu mbinguni na duniani,+ kwa sababu alimwokoa Danieli kutoka katika makucha ya simba.”
-