-
Yoshua 2:9, 10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 Akawaambia: “Najua kwamba Yehova atawapa nchi hii+ na tumeshikwa na hofu kwa sababu yenu.+ Wakaaji wote wa nchi wamevunjika moyo kwa sababu yenu,+ 10 kwa maana tumesikia jinsi Yehova alivyoyakausha maji ya Bahari Nyekundu* mbele yenu mlipotoka Misri+ na mambo mliyowatendea wale wafalme wawili wa Waamori, yaani, Sihoni+ na Ogu,+ waliokuwa ng’ambo ya* Yordani, mliowaangamiza kabisa.
-
-
1 Mambo ya Nyakati 16:24Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
24 Tangazeni utukufu wake miongoni mwa mataifa,
Kazi zake zinazostaajabisha miongoni mwa mataifa yote.
-
-
Isaya 63:12Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
12 Yule aliyeufanya mkono Wake mtukufu uende pamoja na mkono wa kulia wa Musa,+
Yule aliyeyatenganisha maji mbele yao+
Ili kujifanyia jina la milele,+
-