-
Hesabu 21:33, 34Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
33 Halafu wakageuka na kupanda kupitia njia ya Bashani. Ndipo Ogu+ mfalme wa Bashani akatoka pamoja na watu wake wote ili kupigana vita nao huko Edrei.+ 34 Yehova akamwambia Musa: “Usimwogope,+ kwa maana nitamtia mikononi mwako pamoja na watu wake wote na nchi yake,+ nawe utamtendea kama ulivyomtendea Sihoni mfalme wa Waamori, aliyeishi Heshboni.”+
-
-
Kumbukumbu la Torati 3:3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Basi Yehova Mungu wetu akamtia pia mikononi mwetu Mfalme Ogu wa Bashani pamoja na watu wake wote, nasi tukaendelea kumshambulia hivi kwamba hakuna mtu yeyote kati ya watu wake aliyeokoka.
-
-
Yoshua 9:9, 10Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
9 Wakamjibu: “Sisi watumishi wako tumetoka nchi ya mbali sana+ kwa sababu ya heshima ya jina la Yehova Mungu wako, kwa kuwa tumesikia umaarufu wake na mambo yote aliyotenda Misri+ 10 na mambo yote aliyowatendea wale wafalme wawili wa Waamori waliokuwa ng’ambo ya* Yordani, yaani, Mfalme Sihoni+ wa Heshboni na Mfalme Ogu+ wa Bashani, aliyekuwa Ashtarothi.
-