Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hesabu 21:21-24
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 21 Sasa Waisraeli wakawatuma wajumbe wakamwambie hivi Sihoni mfalme wa Waamori:+ 22 “Turuhusu tupite katika nchi yako. Hatutageuka na kuingia katika mashamba yenu au shamba lolote la mizabibu. Hatutakunywa maji ya kisima chochote. Tutafuata Barabara ya Mfalme mpaka tutakapokuwa tumepita katika eneo lako.”+ 23 Lakini Sihoni hakuwaruhusu Waisraeli wapitie katika eneo lake. Badala yake, Sihoni akawakusanya watu wake wote kwenda kuwashambulia Waisraeli nyikani, akafika Yahazi na kuanza kupigana nao.+ 24 Lakini Waisraeli wakamshinda kwa upanga+ na kumiliki nchi yake+ kuanzia Arnoni+ mpaka Yaboki,+ karibu na Waamoni, kwa sababu jiji la Yazeri+ linapakana na eneo la Waamoni.+

  • Kumbukumbu la Torati 2:32-34
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 Sihoni alipotoka na watu wake wote ili kupigana nasi kule Yahazi,+ 33 Yehova Mungu wetu alimtia mikononi mwetu, hivi kwamba tukamshinda yeye, wanawe, na watu wake wote. 34 Tuliteka majiji yake yote wakati huo na kuangamiza kila jiji, pamoja na wanaume, wanawake, na watoto. Hatukumwacha mtu yeyote akiwa hai.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki