-
Kumbukumbu la Torati 2:30-35Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
30 Lakini Mfalme Sihoni wa Heshboni hakuturuhusu tupite, kwa sababu Yehova Mungu wenu alimwacha awe na roho ya ukaidi+ na moyo wake uwe mgumu, ili amtie mikononi mwenu kama ilivyo leo.+
31 “Kisha Yehova akaniambia, ‘Angalieni, tayari nimeanza kumtia mikononi mwenu Sihoni pamoja na nchi yake. Anzeni kuimiliki nchi yake.’+ 32 Sihoni alipotoka na watu wake wote ili kupigana nasi kule Yahazi,+ 33 Yehova Mungu wetu alimtia mikononi mwetu, hivi kwamba tukamshinda yeye, wanawe, na watu wake wote. 34 Tuliteka majiji yake yote wakati huo na kuangamiza kila jiji, pamoja na wanaume, wanawake, na watoto. Hatukumwacha mtu yeyote akiwa hai.+ 35 Tulijichukulia tu mifugo pamoja na nyara za majiji tuliyokuwa tumeteka.
-
-
Waamuzi 11:19, 20Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
19 “‘Kisha Waisraeli wakatuma wajumbe kwa Sihoni mfalme wa Waamori, mfalme wa Heshboni, wakamwambia hivi: “Tafadhali, turuhusu tupitie katika nchi yako twende katika nchi yetu.”+ 20 Lakini Sihoni hakuwaruhusu Waisraeli wapitie katika eneo lake kwa sababu hakuwaamini, basi Sihoni akawakusanya watu wake na kupiga kambi huko Yahazi na kupigana na Waisraeli.+
-