Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kutoka 32:9
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 9 Yehova akaendelea kumwambia Musa: “Nimeona kwamba watu hawa ni wakaidi.*+

  • Kumbukumbu la Torati 1:43
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 43 Basi nikaongea nanyi, lakini hamkusikiliza. Badala yake, mliasi agizo la Yehova na kujaribu kwa kimbelembele kupanda mlimani.

  • Kumbukumbu la Torati 31:27
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 27 Kwa maana mimi mwenyewe najua vizuri uasi wenu+ na ukaidi wenu.*+ Ikiwa mmekuwa mkimwasi sana Yehova ningali hai pamoja nanyi, basi mtamwasi kadiri gani nikifa?

  • 2 Wafalme 17:13, 14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Yehova aliwaonya Waisraeli na watu wa Yuda tena na tena kupitia manabii wake wote na kila mwonaji,+ akisema: “Geukeni na kuacha njia zenu ovu!+ Shikeni amri zangu na maagizo yangu kulingana na sheria yote niliyowaamuru mababu zenu na ambayo niliwapa kupitia watumishi wangu manabii.” 14 Lakini hawakusikiliza, nao wakaendelea kuwa wakaidi kama* mababu zao ambao hawakudhihirisha imani katika Yehova Mungu wao.+

  • Ezekieli 20:18
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 18 Niliwaambia wana wao nyikani,+ ‘Msitembee katika masharti ya mababu zenu+ wala kushika hukumu zao wala kujichafua kwa sanamu zao zinazochukiza.

  • Matendo 7:51
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 51 “Ninyi watu wagumu na wasiotahiriwa katika mioyo na masikio, sikuzote mnaipinga roho takatifu; kama mababu zenu walivyofanya, ndivyo mnavyofanya pia.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki