Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Waamuzi 6:1-5
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Lakini Waisraeli wakatenda tena mambo maovu machoni pa Yehova,+ basi Yehova akawatia mikononi mwa Wamidiani kwa miaka saba.+ 2 Na Wamidiani wakawakandamiza Waisraeli.+ Kwa sababu ya Wamidiani, Waisraeli wakachimba mashimo ya kujificha* katika milima, mapango, na mahali pagumu kufikiwa.+ 3 Waisraeli walipopanda mbegu, Wamidiani, Waamaleki,+ na watu wa Mashariki+ waliwashambulia. 4 Nao walikuwa wakipiga kambi ili kuwashambulia na kuharibu mazao yote nchini hadi Gaza, na hawakuwaachia Waisraeli chakula chochote, wala kondoo, ng’ombe dume, au punda.+ 5 Walikuja na mifugo yao na mahema mengi sana kama nzige,+ na wao pamoja na ngamia wao hawangeweza kuhesabiwa,+ walikuja ili kuiharibu nchi.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki