7 Moyo wangu uko imara, Ee Mungu,+
Moyo wangu uko imara.
Nitaimba na kupiga muziki.
8 Amka, utukufu wangu.
Amka, Ee kinanda; nawe pia, Ee kinubi.
Nitayaamsha mapambazuko.+
9 Nitakusifu miongoni mwa mataifa, Ee Yehova;+
Nitakuimbia sifa miongoni mwa mataifa.+
10 Kwa maana upendo wako mshikamanifu ni mkubwa, uko juu kama mbingu,+
Na uaminifu wako, unafika mpaka angani.
11 Ukwezwe juu ya mbingu, Ee Mungu;
Utukufu wako na uwe juu ya dunia yote.+