9 Ni nani atakayenipeleka kwenye jiji lililozingirwa?
Ni nani atakayeniongoza mpaka Edomu?+
10 Je, si wewe, Ee Mungu, ambaye umetukataa,
Mungu wetu, ambaye haendi tena na majeshi yetu?+
11 Tusaidie katika taabu yetu,
Kwa maana wokovu kutoka kwa wanadamu hauna faida yoyote.+
12 Kwa msaada wa Mungu tutapata nguvu,+
Naye atawakanyagia chini maadui wetu.+