-
Ufunuo 8:3, 4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Malaika mwingine, akiwa ameshika chombo cha uvumba* cha dhahabu,+ akafika na kusimama kwenye madhabahu, naye akapewa kiasi kikubwa cha uvumba+ ili autoe pamoja na sala za watakatifu wote juu ya madhabahu ya dhahabu+ ambayo ilikuwa mbele ya kile kiti cha ufalme. 4 Moshi wa uvumba kutoka kwenye mkono wa huyo malaika ukapanda pamoja na sala+ za watakatifu mbele za Mungu.
-