-
2 Wafalme 6:15, 16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Mtumishi* wa mtu wa Mungu wa kweli alipoamka asubuhi na mapema na kutoka nje, aliona jeshi lenye farasi na magari ya vita yakiwa yamezunguka jiji. Mara moja mtumishi huyo akamwambia: “Ole wetu, bwana wangu! Tutafanya nini?” 16 Lakini Elisha akamwambia: “Usiogope!+ Kwa maana wale walio pamoja nasi ni wengi kuliko wale walio pamoja nao.”+
-
-
Zaburi 27:3Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
Hata vita vikizuka dhidi yangu,
Bado nitaendelea kuwa jasiri.
-