70 Ee Mungu, niokoe;
Ee Yehova, njoo haraka unisaidie.+
 2 Wale wanaotaka kuniua
Na waaibishwe na kufedheheshwa.
Wale wanaofurahia msiba wangu
Na wakimbie kwa aibu.
 3 Wale wanaosema: “Aha! Aha!”
Na wakimbizwe kwa aibu.
 4 Lakini acha wale wanaokutafuta
Wafurahi na kushangilia kwa sababu yako.+
Wale wanaopenda matendo yako ya wokovu na waseme daima:
“Mungu na atukuzwe!”
 5 Lakini sina uwezo, nami ni maskini;+
Ee Mungu, tenda haraka kwa niaba yangu.+
Wewe ni msaidizi wangu na mwokozi wangu.+
Ee Yehova, usikawie.+