-
Isaya 63:11-13Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
11 Nao wakazikumbuka siku za zamani,
Siku za Musa mtumishi wake:
“Yuko wapi Yule aliyewapandisha kutoka katika bahari+ pamoja na wachungaji wa kundi lake?+
Yuko wapi Yule aliyetia ndani yake roho Yake takatifu,+
12 Yule aliyeufanya mkono Wake mtukufu uende pamoja na mkono wa kulia wa Musa,+
Yule aliyeyatenganisha maji mbele yao+
Ili kujifanyia jina la milele,+
13 Yule aliyewafanya watembee katika maji yenye mawimbi makubwa,*
Hivi kwamba wakatembea bila kujikwaa,
Kama farasi katika nchi iliyo wazi?*
-