13 Mwanamke mpumbavu ana kelele.+
Yeye ni mjinga na hajui chochote.
14 Huketi kwenye mlango wa nyumba yake
Kwenye kiti sehemu zilizoinuka jijini,+
15 Akiwaita kwa sauti wale wanaopita karibu naye,
Waendao moja kwa moja kwenye njia yao:
16 “Yeyote ambaye ni mjinga, aje hapa.”
Huwaambia wale wasio na busara:+
17 “Maji yaliyoibwa ni matamu,
Na chakula kinacholiwa sirini kinapendeza.”+
18 Lakini hawajui kwamba wale waliokufa ambao hawana uwezo wako hapo,
Na kwamba wageni wake wamo katika vina vya Kaburi.+