8 “Mtu akikualika kwenye karamu ya ndoa, usiketi mahali pa heshima zaidi.+ Huenda pia amemwalika mtu mashuhuri kuliko wewe. 9 Naye aliyewaalika atakuja kukuambia, ‘Mwachie mtu huyu mahali ulipoketi.’ Kisha utaondoka kwa aibu na kuketi mahali pa chini kabisa.