Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 11:6, 7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 6 Ndipo Yehova akasema: “Tazama! Watu hawa ni kitu kimoja na wanazungumza lugha moja,+ na hili ndilo jambo waliloanza kufanya. Sasa hakuna jambo lolote wanalokusudia kufanya litakalowashinda. 7 Njooni! Tushuke+ huko na kuvuruga lugha yao ili kila mmoja wao asiielewe lugha ya mwenzake.”

  • Mwanzo 50:19, 20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Yosefu akawaambia: “Msiogope. Je, nimechukua nafasi ya Mungu? 20 Ingawa mlikusudia kunidhuru,+ Mungu alikusudia hali hiyo ibadilike na kuwa njema na kuokoa maisha ya watu wengi, kama anavyofanya leo.+

  • Methali 21:30
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 30 Hakuna hekima, wala utambuzi wowote, wala shauri katika kumpinga Yehova.+

  • Danieli 4:35
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 35 Wakaaji wote wa dunia wanaonwa kuwa si kitu, naye hufanya kulingana na mapenzi yake mwenyewe miongoni mwa jeshi la mbinguni na wakaaji wa dunia. Na hakuna yeyote anayeweza kumzuia*+ au kumuuliza, ‘Umefanya nini?’+

  • Matendo 5:38, 39
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 38 Basi chini ya hali zilizopo, ninawaambia, msiingilie mambo ya watu hawa, bali waacheni. Kwa maana, ikiwa mpango huu au kazi hii ni ya wanadamu, itaangamizwa; 39 lakini ikiwa imetoka kwa Mungu, hamtaweza kuwaangamiza.+ La sivyo, huenda ikawa mnapigana na Mungu mwenyewe.”+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki