Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Mwanzo 9:20, 21
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 Sasa Noa akaanza kulima, akapanda shamba la mizabibu. 21 Alipokunywa divai, alilewa, naye akavua nguo ndani ya hema lake.

  • Methali 23:29-35
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 29 Ni nani mwenye ole? Ni nani aliye na wasiwasi?

      Ni nani mwenye ugomvi? Ni nani anayelalamika?

      Ni nani aliye na majeraha bila sababu? Ni nani aliye na macho mazito?*

      30 Ni wale wanaoshinda kwenye divai;+

      Wale wanaotafuta* divai iliyochanganywa.

      31 Usiitazame rangi nyekundu ya divai

      Inapong’aa katika kikombe na kushuka taratibu,

      32 Kwa maana mwishowe huuma kama nyoka,

      Nayo hutoa sumu kama nyoka kipiri.

      33 Macho yako yataona mambo ya ajabu,

      Na moyo wako utasema mambo yaliyopotoka.+

      34 Nawe utakuwa kama mtu anayelala katikati ya bahari,

      Kama mtu anayelala juu ya mlingoti wa meli.

      35 Utasema: “Wamenipiga, lakini sikuhisi chochote.*

      Walinipiga, lakini sikujua.

      Nitaamka lini?+

      Nahitaji kinywaji kingine.”*

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki