5 Katika siku za Herode,+ mfalme wa Yudea, kulikuwa na kuhani aliyeitwa Zekaria wa kikundi cha Abiya.+ Mke wake aliitwa Elisabeti na alikuwa wa ukoo wa Haruni. 6 Wote wawili walikuwa waadilifu mbele za Mungu na walitembea bila lawama kulingana na amri na sheria zote za Yehova.