11 Ole wao wanaoamka asubuhi na mapema ili wanywe kileo,+
Wanaokawia hadi giza linapoingia jioni mpaka divai inapowawasha!
12 Wana kinubi na kinanda,
Tari, filimbi, na divai katika karamu zao;
Lakini hawafikirii utendaji wa Yehova,
Wala hawaioni kazi ya mikono yake.