-
1 Wafalme 18:24, 25Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
24 Kisha mtaliita jina la mungu wenu,+ nami nitaliita jina la Yehova. Mungu atakayejibu kwa moto, atathibitisha kwamba yeye ndiye Mungu wa kweli.”+ Ndipo watu wote wakasema: “Jambo unalosema ni jema.”
25 Sasa Eliya akawaambia manabii wa Baali: “Chagueni ng’ombe dume mmoja mchanga na kumtayarisha kwanza, kwa sababu ninyi ni wengi. Kisha mliite jina la mungu wenu, lakini msiwashe moto.”
-