-
Isaya 45:1, 2Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
45 Hivi ndivyo Yehova anavyomwambia mtiwa-mafuta wake, Koreshi,+
Ambaye nimeushika mkono wake wa kulia+
Ili kuyatiisha mataifa mbele yake,+
Kuwanyang’anya silaha* wafalme,
Kufungua mbele yake milango yenye pande mbili,
Hivi kwamba malango hayatafungwa:
Nitaivunja milango ya shaba vipandevipande,
Nami nitayakata makomeo ya chuma.+
-