-
Kutoka 20:4, 5Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
4 “Usijitengenezee sanamu ya kuchongwa au mfano wa* kitu chochote kilicho juu mbinguni au kilicho chini duniani au kilicho ndani ya maji chini ya dunia.+ 5 Usiviinamie wala kushawishiwa kuviabudu,+ kwa sababu mimi, Yehova Mungu wako, ni Mungu ninayetaka watu waniabudu mimi peke yangu,+ nami huwaadhibu watoto kwa sababu ya makosa ya baba zao, kufikia kizazi cha tatu na kizazi cha nne cha wale wanaonichukia,
-
-
Habakuki 2:18, 19Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
18 Sanamu ya kuchongwa ina faida gani
Na mtu ndiye aliyeichonga?
Sanamu ya chuma* na mwalimu wa uwongo ana faida gani,
Hata ingawa yule aliyeitengeneza anaitumaini,
Akitengeneza miungu ya ubatili ambayo haiwezi kuongea?+
19 Ole wake anayekiambia kipande cha ubao, “Amka!”
Au anayeliambia jiwe lisiloweza kuongea, “Amka! Tufundishe!”
-