-
Nehemia 9:30, 31Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
30 Uliwaonyesha subira+ kwa miaka mingi na ukaendelea kuwaonya kwa roho yako kupitia manabii wako, lakini walikataa kusikiliza. Mwishowe ukawatia mikononi mwa mataifa ya nchi hizo.+ 31 Na kwa sababu ya rehema zako nyingi, hukuwaangamiza+ wala kuwaacha, kwa maana wewe ni Mungu mwenye huruma* na rehema.+
-
-
Zaburi 78:38Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
Mara nyingi aliizuia hasira yake+
Badala ya kuichochea ghadhabu yake yote.
-