-
Yeremia 34:15, 16Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
15 Na hivi karibuni* ninyi wenyewe mligeuka na kufanya yaliyo sawa machoni pangu kwa kuwatangazia uhuru wenzenu, nanyi mkafanya agano mbele zangu katika nyumba inayoitwa kwa jina langu. 16 Lakini mligeuka tena na kulichafua jina langu+ kwa kuwarudisha watumwa wenu wa kiume na wa kike ambao mlikuwa mmewaachilia huru kama walivyotaka, nanyi mkawalazimisha tena kuwa watumwa.’
-
-
Mika 3:2-4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
2 Lakini mnachukia mema+ na kupenda maovu;+
Mnawachuna ngozi watu wangu na kuondoa nyama kutoka kwenye mifupa yao.+
3 Pia mnakula nyama ya watu wangu+
Na kuwachuna ngozi,
Mnapasua mifupa yao, na kuivunja vipandevipande,+
Kama kitu kinachopikwa ndani ya chungu,* kama nyama ndani ya chungu cha kupikia.
4 Wakati huo watamlilia Yehova awasaidie,
Lakini hatawajibu.
-