Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 5:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  7 Kwa maana shamba la mizabibu la Yehova wa majeshi ni nyumba ya Israeli;+

      Watu wa Yuda ndilo shamba alilolipenda sana.

      Aliendelea kutumaini haki itendwe,+

      Lakini tazama! kulikuwa na ukosefu wa haki;

      Alitumaini uadilifu ufanywe,

      Lakini tazama! kulikuwa na kilio cha huzuni.”+

  • Isaya 59:15
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 15 Ukweli* umetoweka,+

      Na yeyote anayeacha ubaya anaporwa.

      Yehova aliona jambo hilo naye akachukizwa,*

      Kwa maana hakukuwa na haki.+

  • Yeremia 5:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 5 Tembeeni huku na huku katika barabara za Yerusalemu.

      Tazameni pande zote mwone.

      Tafuteni katika viwanja vyake vya jiji

      Ikiwa mnaweza kumpata mtu anayetenda haki,+

      Yeyote anayejitahidi kuwa mwaminifu,

      Nami nitalisamehe jiji hilo.

  • Amosi 6:12
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 12 Je, farasi hukimbia kwenye mwamba,

      Au je, mtu anaweza kulima kwa ng’ombe kwenye mwamba?

      Kwa maana mmebadili haki kuwa mmea wenye sumu,

      Na tunda la uadilifu kuwa pakanga.*+

  • Habakuki 1:4
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  4 Kwa hiyo sheria haifanyi kazi,

      Na haki haitekelezwi kamwe.

      Kwa maana mwovu amemzingira mwadilifu;

      Ndiyo sababu haki imepotoshwa.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki