Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 18:13, 14
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Katika mwaka wa 14 wa utawala wa Mfalme Hezekia, Senakeribu mfalme wa Ashuru+ alipanda kuja kuyashambulia majiji yote yenye ngome ya Yuda na kuyateka.+ 14 Kwa hiyo Mfalme Hezekia wa Yuda akatuma ujumbe huu kwa mfalme wa Ashuru kule Lakishi: “Nimekosea. Ondokeni, msinishambulie, nami nitalipa chochote mtakachonitoza.” Mfalme wa Ashuru akamtoza Mfalme Hezekia wa Yuda faini ya talanta 300 za fedha* na talanta 30 za dhahabu.

  • Isaya 8:7, 8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  7 Kwa hiyo tazama! Yehova ataleta dhidi yao

      Maji yenye nguvu na yaliyo mengi ya ule Mto,*

      Mfalme wa Ashuru+ na utukufu wake wote.

      Atakuja juu ya sakafu zake zote za vijito

      Na kufurika kwenye kingo zake zote

       8 Na kupita katika nchi yote ya Yuda.

      Atafurika na kuvuka, na kufika shingoni;+

      Mabawa yake yaliyonyooshwa yatajaza upana wa nchi yako,

      Ewe Imanueli!”*+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki