Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Mambo ya Nyakati 28:19, 20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 19 Yehova aliwanyenyekeza watu wa Yuda kwa sababu ya Mfalme Ahazi wa Israeli, kwa maana aliwaacha watu wa Yuda watende watakavyo, na hivyo wakakosa kuwa waaminifu kwa Yehova kwa kiwango kikubwa.

      20 Hatimaye Mfalme Tilgath-pilneseri+ wa Ashuru akaja kukabiliana naye na kumtesa+ badala ya kumtia nguvu.

  • Isaya 7:17
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 17 Yehova ataleta dhidi yako na dhidi ya watu wako na dhidi ya nyumba ya baba yako wakati ambao haujawahi kuonekana tangu Efraimu lilipojitenga na Yuda,+ kwa maana Yeye atamleta mfalme wa Ashuru.+

  • Isaya 7:20
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 20 “Siku hiyo, kwa kutumia wembe uliokodiwa kutoka eneo la ule Mto,* kwa kumtumia mfalme wa Ashuru,+ Yehova atanyoa kichwa na nywele za miguu, nao utafagilia mbali ndevu pia.

  • Isaya 10:28-32
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 Amekuja Aiathi;+

      Amepitia Migroni;

      Ameweka mizigo yake huko Mikmashi.+

      29 Wamevuka kivuko;

      Wamekaa Geba usiku kucha;+

      Rama inatetemeka, Gibea+ ya Sauli imekimbia.+

      30 Paza sauti yako na upige mayowe, Ee binti ya Galimu!

      Sikiliza, Ee Laisha!

      Ewe maskini Anathothi!+

      31 Madmena amekimbia.

      Wakaaji wa Gebimu wametafuta mahali pa kujificha.

      32 Leo hiihii atasimama Nobu.+

      Anautikisia ngumi mlima wa binti ya Sayuni,

      Kilima cha Yerusalemu.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki