Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Isaya 35:10
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 Wale waliokombolewa na Yehova watarudi+ na kuja Sayuni kwa kilio cha shangwe.+

      Shangwe isiyo na kikomo itakuwa taji la vichwa vyao.+

      Watapata shangwe na furaha,

      Na huzuni na kilio cha uchungu vitatoweka.+

  • Isaya 61:7
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  7 Badala ya aibu mtakuwa na fungu mara mbili,

      Na badala ya fedheha watapiga vigelegele kwa shangwe kwa sababu ya fungu lao.

      Naam, watamiliki fungu mara mbili katika nchi yao.+

      Watakuwa na shangwe milele.+

  • Yeremia 33:10, 11
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 10 “Yehova anasema hivi, ‘Mahali hapa ambapo mtasema ni nchi iliyo ukiwa, isiyo na wanadamu wala mifugo, katika majiji ya Yuda na katika barabara za Yerusalemu zilizo tupu, bila wanadamu wala wakaaji wala mifugo, itasikika tena 11 sauti ya furaha na sauti ya shangwe,+ sauti ya bwana harusi na sauti ya bibi harusi, sauti ya wale wanaosema: “Mshukuruni Yehova wa majeshi, kwa maana Yehova ni mwema;+ upendo wake mshikamanifu unadumu milele!”’+

      “‘Wataleta matoleo ya shukrani katika nyumba ya Yehova,+ kwa maana nitawarudisha mateka wa nchi, kama hapo mwanzoni,’ asema Yehova.”

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki