6 Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea, mfalme wa Ashuru aliliteka jiji la Samaria.+ Kisha akawapeleka Waisraeli uhamishoni+ kule Ashuru na kuwaweka katika eneo la Hala na Habori kando ya mto Gozani+ na katika majiji ya Wamedi ili waishi humo.+
6 Gomeri akapata mimba tena na kuzaa binti. Mungu akamwambia Hosea: “Mpe binti huyo jina Lo-ruhama,* kwa maana sitaionyesha tena rehema+ nyumba ya Israeli, kwa sababu kwa hakika nitawafukuza.+