“Wakati wa kibali nilikujibu,+
Na katika siku ya wokovu nilikusaidia;+
Niliendelea kukulinda ili nikutoe uwe agano kwa ajili ya watu,+
Ili kuitengeneza upya nchi,
Ili kuwafanya wamiliki urithi wao ulio ukiwa,+
-
Isaya 51:3
Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Kwa maana Yehova atalifariji Sayuni.+
Ataleta faraja kwa magofu yake yote,+
Naye ataifanya nyika yake kuwa kama Edeni+
Na jangwa lake tambarare kama bustani ya Yehova.+
Kutakuwa na furaha na shangwe ndani yake,
Kutoa shukrani na nyimbo tamu.+