12 Kwa maana nitapita katikati ya nchi ya Misri usiku huo na kumuua kila mzaliwa wa kwanza katika nchi ya Misri, kuanzia mwanadamu mpaka mnyama;+ nami nitatekeleza hukumu dhidi ya miungu yote ya Misri.+ Mimi ni Yehova.
12 Nami nitaziwasha moto nyumba za* miungu ya Misri,+ naye ataiteketeza na kuichukua mateka. Atajifunika kwa nchi ya Misri kama mchungaji anavyojifunika kwa vazi lake, naye ataondoka huko kwa amani.*
25 “Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: ‘Sasa ninamkazia fikira Amoni+ kutoka No,*+ Farao, Misri, miungu yake,+ wafalme wake—naam, Farao na wote wanaomtumaini.’+
13 “Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova anasema hivi: ‘Nitaziangamiza pia sanamu zinazochukiza* na kuiharibu miungu ya ubatili ya Nofu.*+ Hakutakuwa tena na mkuu* anayetoka katika nchi ya Misri, nami nitaweka hofu katika nchi ya Misri.+