-
Waamuzi 17:3, 4Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
3 Basi akamrudishia mama yake vile vipande 1,100 vya fedha, lakini mama yake akasema, “Nitazitakasa fedha hizi kwa ajili ya Yehova zitoke mikononi mwangu ili mwanangu azitumie kutengeneza sanamu ya kuchongwa na sanamu ya chuma.*+ Sasa nakurudishia fedha hizi.”
4 Baada ya kumrudishia mama yake fedha hizo, mama yake akachukua vipande 200 vya fedha na kumpa mfua fedha. Naye akatengeneza sanamu ya kuchongwa na sanamu ya chuma;* na sanamu hizo zikawekwa katika nyumba ya Mika.
-