Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • 2 Wafalme 18:13
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 13 Katika mwaka wa 14 wa utawala wa Mfalme Hezekia, Senakeribu mfalme wa Ashuru+ alipanda kuja kuyashambulia majiji yote yenye ngome ya Yuda na kuyateka.+

  • 2 Mambo ya Nyakati 32:1
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 32 Baada ya mambo hayo na matendo hayo ya uaminifu,+ Mfalme Senakeribu wa Ashuru alikuja na kuvamia Yuda. Alizingira majiji yenye ngome, akikusudia kuvunja na kuingia ndani na kuyateka.+

  • Isaya 8:7, 8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  7 Kwa hiyo tazama! Yehova ataleta dhidi yao

      Maji yenye nguvu na yaliyo mengi ya ule Mto,*

      Mfalme wa Ashuru+ na utukufu wake wote.

      Atakuja juu ya sakafu zake zote za vijito

      Na kufurika kwenye kingo zake zote

       8 Na kupita katika nchi yote ya Yuda.

      Atafurika na kuvuka, na kufika shingoni;+

      Mabawa yake yaliyonyooshwa yatajaza upana wa nchi yako,

      Ewe Imanueli!”*+

  • Isaya 10:28-32
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    • 28 Amekuja Aiathi;+

      Amepitia Migroni;

      Ameweka mizigo yake huko Mikmashi.+

      29 Wamevuka kivuko;

      Wamekaa Geba usiku kucha;+

      Rama inatetemeka, Gibea+ ya Sauli imekimbia.+

      30 Paza sauti yako na upige mayowe, Ee binti ya Galimu!

      Sikiliza, Ee Laisha!

      Ewe maskini Anathothi!+

      31 Madmena amekimbia.

      Wakaaji wa Gebimu wametafuta mahali pa kujificha.

      32 Leo hiihii atasimama Nobu.+

      Anautikisia ngumi mlima wa binti ya Sayuni,

      Kilima cha Yerusalemu.

  • Isaya 33:8
    Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
    •  8 Barabara kuu zimebaki tupu;

      Hakuna mtu anayesafiri kwenye vijia.

      Amelivunja* agano;

      Ameyakataa majiji;

      Hamheshimu mwanadamu anayeweza kufa.+

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki