-
2 Wafalme 18:17, 18Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Kisha mfalme wa Ashuru akamtuma Tartani,* Rabsarisi,* na Rabshake* pamoja na jeshi kubwa kutoka Lakishi+ kwenda kwa Mfalme Hezekia kule Yerusalemu.+ Wakapanda kwenda Yerusalemu na kujipanga karibu na mfereji wa kidimbwi cha juu, kwenye barabara kuu ya uwanja wa mfuaji wa nguo.+ 18 Walipomwita mfalme atoke nje, Eliakimu+ mwana wa Hilkia, aliyekuwa msimamizi wa nyumba,* Shebna+ aliyekuwa mwandishi, na Yoa mwana wa Asafu aliyefanya kazi ya kuweka kumbukumbu, wakaenda nje kukutana nao.
-