30 Nawe usikilize ombi langu mimi mtumishi wako la kutaka kibali na pia ombi ambalo watu wako Waisraeli wanaomba kuelekea mahali hapa, nawe usikilize katika makao yako mbinguni;+ naam, usikilize na kusamehe.+
20 Macho yako na yatazame nyumba hii usiku na mchana, yatazame mahali ambapo ulisema kwamba utaweka jina lako,+ ili usikilize sala ambayo mimi mtumishi wako ninasali kuelekea mahali hapa.
9 ‘Tukipatwa na msiba, upanga, hukumu kali, au ugonjwa hatari, au njaa, na tusimame mbele ya nyumba hii na mbele zako (kwa maana jina lako limo katika nyumba hii)+ na kukulilia utusaidie katika taabu yetu, nawe usikie na kutuokoa.’+