-
2 Wafalme 19:29-31Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
29 “‘Na hii ndiyo itakayokuwa ishara kwako:* Mwaka huu utakula mimea inayoota yenyewe;* na katika mwaka wa pili utakula nafaka inayochipuka kutoka katika mimea hiyo;+ lakini katika mwaka wa tatu utapanda mbegu na kuvuna, nawe utapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake.+ 30 Watu wa nyumba ya Yuda watakaoponyoka, wale wanaobaki,+ watatia mizizi chini na kuzaa matunda kwenda juu. 31 Kwa maana waliobaki watatoka Yerusalemu na waokokaji watatoka katika Mlima Sayuni. Bidii ya Yehova wa majeshi itatenda hayo.+
-