-
Yoshua 4:21-24Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
21 Akawaambia hivi Waisraeli: “Watoto wenu watakapowauliza wakati ujao, ‘Mawe haya ni ya nini?’+ 22 Waambieni, ‘Waisraeli walivuka katikati ya Mto Yordani kwenye nchi kavu+ 23 Yehova Mungu wenu alipoyakausha maji ya Yordani mbele yao mpaka walipovuka, kama Yehova Mungu wenu alivyoikausha Bahari Nyekundu* mbele yetu mpaka tulipovuka.+ 24 Alifanya hivyo ili watu wote duniani wajue jinsi mkono wa Yehova ulivyo na nguvu+ na ili ninyi mmwogope Yehova Mungu wenu sikuzote.’”
-