-
Mambo ya Walawi 25:39-42Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
39 “‘Ikiwa ndugu yako anayeishi karibu nawe amelazimika kujiuza kwako+ kwa sababu amekuwa maskini, usimlazimishe akutumikie kama mtumwa.+ 40 Unapaswa kumtendea kama kibarua,+ kama mhamiaji. Atakutumikia mpaka wakati wa Mwadhimisho wa Miaka 50. 41 Kisha atakuacha, yeye na watoto* wake, na kurudi kwa watu wake wa ukoo. Anapaswa kurudi kwenye urithi wa mababu zake.+ 42 Kwa maana wao ni watumwa wangu niliowatoa nchini Misri.+ Hawapaswi kujiuza kama mtumwa anavyouzwa.
-