-
2 Wafalme 24:17-19Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
17 Mfalme wa Babiloni alimweka Matania, mjomba wa Yehoyakini,+ kuwa mfalme baada yake na kubadili jina lake kuwa Sedekia.+
18 Sedekia alikuwa na umri wa miaka 21 alipoanza kutawala, naye alitawala kwa miaka 11 huko Yerusalemu. Mama yake aliitwa Hamutali+ binti ya Yeremia kutoka Libna. 19 Sedekia aliendelea kutenda maovu machoni pa Yehova, alitenda mambo yote ambayo Yehoyakimu alitenda.+
-