-
Yeremia 49:19-21Biblia Takatifu—Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
-
-
19 “Tazameni! Kama simba anayetoka kwenye vichaka+ vikubwa kando ya Yordani, mtu fulani atayashambulia malisho yaliyo salama, lakini kwa muda mfupi nitamfanya Edomu akimbie kutoka nchini. Nami nitaweka juu ya nchi hiyo yule aliyechaguliwa. Kwa maana ni nani aliye kama mimi, na ni nani atakayenipinga? Ni mchungaji gani anayeweza kusimama mbele zangu?+ 20 Kwa hiyo sikieni, enyi watu, uamuzi ambao* Yehova amefanya dhidi ya Edomu na mawazo yake dhidi ya wakaaji wa Temani:+
Hakika walio wadogo katika kundi watakokotwa.
Atayafanya makao yao yawe ukiwa kwa sababu yao.+
21 Dunia imetetemeka kwa sauti ya kuanguka kwao.
Kuna kilio kikubwa!
Sauti imesikika mpaka kwenye Bahari Nyekundu.+
-